Usafi wa Kucha za Mtoto

Kucha za mtoto mchanga zinakua haraka sana, inawezekana ukahitajika kuzikata karibia mara 2 hadi 3 kwa wiki. Kucha za miguuni hazihitaji kukatwa mara kwa mar asana.

Ujanja ni kununua vifaa safi na maalumu kumkatia mtoto kucha. Unaweza ukanunua kikatio kucha maalumu kwa watoto. Mmoja anaweza akamshika mtoto asiweze kuhangaika sana huku mwingine akimkata kucha zake kwa makini kwani ngozi ya mtoto ni laini sana. Unaweza ukajaribu kumkata kucha akiwa ananyonya au akiwa amelala kupata urahisi zaidi.

Wakati wa kukata kucha elekeza kikatio kucha mbali na mtoto na kuwa makini usikate ngozi yake. Shikilia kwa nguvu kidole cha mtoto wako ukiwa unakata ili kisitingishike na kumkata bahati mbaya. Kama una wasiwasi sana kwamba unaweza ukamkata mtoto, tumia kikwaruzo kucha badala yake na uwe unazikwaruza kucha taratibu sana kwani ukitumia nguvu na kucha zake ni laini unaweza ukapitiliza na kukwaruza ngozi yake laini.

Kama mtoto wako anajikwarua usoni pamoja na kwamba kucha zake ni fupi, unaweza kumvalisha “gloves” au nguo zenye mikono mirefu inayopitiliza vidole.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.