Usafi na Uangalizi wa Kibana Kitovu

Baada ya mtoto wako kuzaliwa, mrija wa chakula toka kwa mama utakatwa na kubanwa na kibana kitovu.

Mfunge nepi mtoto wako ikiwa chini ya kitovu, ili kibana kitovu kipate hewa na pia kisipate mkojo. Epuka kumuogesha mtoto wako mpaka kibana kitovu kitakapodondoka.

Hakikisha kibana kitovu kinakuwa safi kadiri uwezavyo kwa muda wote kitakapokuwa kinakauka mpaka kudondoka, mara nyingi kuanzia siku 10 hadi 21. Kikishadondoka kitaacha kijidonda kidogo kibichi kwenye kitovu ambacho kitapona baada ya siku chache zijazo.

Katika maeneo yenye joto au katika kipindi cha joto ni vyema kumuacha mtoto wako akiwa amevaa nepi na T-shirt kubwa kubwakuruhusu hewa kuingia kwani itasaidia kupona kwa kitovu chake. Epuka kumvalisha mtoto wako nguo zenye kubana sana mpaka pale kibana kitovu kitakapodondoka.

Katika kipindi hiki ukisubiria kibana kitovu kidondoke na kitovu cha mtoto wako kupona kabisa, unaweza ukawa unamsafisha kwa kumfuta na kitambaa laini chenye maji ya vuguvugu ukiwa makini kutokuweka maji kwenye kitovu.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.