Ujauzito Wiki ya 29

Jinsi mtoto wako anavyokua katika ujauzito wiki ya 29
Ubongo wa mtoto wako unakua kwa kasi, na kichwa chake kinakua kikubwa ili kumudu ubongo huo. Kama wewe unatarajia mtoto wa kiume, korodani zake zinasoge kutoka eneo lake zilipo karibu na chini ya figo zake kuelekea chini sehemu yake. Kama unatarajia kupata mtoto wa kike, kinembe chake bado ni kikubwa na kinaonekana sana kwa sababumidomo yake ya uke (labia)bado ni ndogo kuweza kukifunika. Hii itatokea katika wiki chache za mwisho kabla ya kuzaliwa.

Dalili za ujauzito katika wiki ya 29
Hamu yako ya kula huongezeka kulingana na ukuaji wa mtoto wako katika miezi mitatu ya mwisho, hamu hii inaweza ikawa zaidi katika keki, pipi na vyakula vya haraka “fast foods”. Jaribu kula vitu hivi mara chache chache zaidi kuliko mara kwa mara.

Kula vizuri katika hatua hii ya ujauzito ni muhimu kwa afya yako na afya ya mtoto wako. Jaribu kula chakula kingichenye wingi wa chuma, ambayo husaidia kutengeneza seli nyekundu za damu. Mtoto wako atachukua hifadhi ya chuma kutoka mwilinimwako, ili asipungukiwe ila wewe unaweza pungukiwa na kukuletea matatizo.

Ongeza madini ya chuma kwa kula milo yenye vyanzo vya chuma, kama vile nyama isiyo na mafuta,mbogamboga na matunda katika mlo wako.

Sasa ni wakati mzuri wa kujifunza baadhi ya mazoezi ya kujinyoosha ambayo yatafungua mwili wako tayari kwa kuzaa mtoto wako. Usijali kama ni vigumu kwako kujifunza mazoezi mpya. Hata kunyoosha mara kwa mara inaweza kukusaidia kuepuka misuli kubana na kuvimba miguu.

Unachotakiwa kufahamu katika ujauzito wiki ya 29
Sasa ni wakati mzuri wa kujifunza baadhi ya mazoezi ya kujinyoosha ambayo yatafungua mwili wako tayari kwa kuzaa mtoto wako. Usijali kama ni vigumu kwako kujifunza mazoezi mpya. Hata kunyoosha mara kwa mara inaweza kukusaidia kuepuka misuli kubana na kuvimba miguu.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.