Ni Nini cha Kufanya Mtoto Anapocheua

Mtoto wako inabidi acheue kwa sababu huwa anachukua hewa nyingi akiwa ananyonya. Kupunguza kiasi cha hewa anachokiingiza tumboni wakati ananyonya hakikisha yupo kwenye mkao sahihi wa kunyonya na na chuchu imeingia vizuri mdomoni. Midomo yake inabidi iwe imeifunika kabisa chuchu au chupa ya maziwa bila kuacha nafasi wakati ananyonya.

Muweke mtoto wako mabegani mwako. Simama au kaa vizuri, ukiwa umeegemea nyuma kidogo, mshikilie mtoto kwa matakoni ili umbebe vizuri. Hakikisha anaangalia nyuma yako kupitia moja ya mabega yako, kidevu chake kikiwa kimeegemea kwenye kitambaa safi ili kama akicheua usichafuke.

Mpige pige taratibu mgongoni. Msugue kwa mwendo wa chini juu chini juu mgongoni kwake karibu na mabega yake. Kuwa mvumilivu: Inaweza kuchukua dakika 4 hadi 5 mpaka mtoto wako acheue. Hakikisha unaagalia kichwa cha mtoto wako. Watoto wengine hukisukuma kichwa chao nyuma kwa ghafla na kama hakijashikiliwa vizuri anaweza akajiumiza.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.