Mikao Mbalimbali Wakati wa Uchungu

Baadhi ya mikao ambayo unaweza kujaribu ni pamoja na:

  1. Kusimama
  2. Kutembea tembea kadiri uwezavyo
  3. Kukaa
  4. Kuchuchumaa na kuegemea kiti, kitanda au mwenza wako
  5. Kupiga magoti na kuegemea mahali
  6. Kutambaa (Inaweza ikapunguza maumivu makali ya mgongo)

Kama mikao yote hii inakuletea shida na haisaidii na unaona kujilaza kwa mgongo ndio husaidia, jaribu kulala upande upande ukiwa umeweka mto kukusaidia. Vile vile kama ulivyokuwa unalala katika miezi 6 iliyopita.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.