Mbinu za Kupumua Kipindi cha Uchungu

Kujifunza mbinu za upumuaji zitakazokusaidia wakati wa uchungu ni jambo zuri kwani itakusaidia kuwa makini, kukabiliana na maumivu ya mkazo nyonga, kusaidia uchungu kwenda haraka, na pia kuhifadhi nguvu zako mpaka wakati wa kusukuma.

Wakati unahudhuria kliniki utakuwa umefundishwa mbinu mbali mbali za upumuaji, ikiwemo:

  1. Kuvuta pumzi taratibu ndani na kuitoa nje
  2. Vuta pumzi ndani kwa kutumia pua na utoe pumzi kwa mdomo, hesabu mpaka tatu unapovuta pumzi ndani na pia hesabu mpaka tatu wakati unatoa pumzi nje
  3. Kupumua haraka haraka husaidia wakati wa kusukuma, ukiupa uke wako nafasi ya kujinyoosha wakati mtoto anapita kwenye njia ya kujifungulia.

Kufanya mazoezi haya ya kupumua na mwenza wako mapema ni njia nzuri ya kujitayarisha kwa uchungu.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.