Mazoezi ya Sakafu ya Nyonga kwa Mjamzito

Moja ya zoezi unaloweza kujumuisha na mazoezi yako ya kila siku wakati ukiwa na mimba ni mazoezi ya sakafu ya nyonga. Moja ya mambo mazuri juu ya haya mazoezi ni kwamba, ni wewe peke yako ndio utakayejua unayafanya. Hii inamaanisha unaweza kufanya wakati umekaa kwenye meza, wakati ukiwa kwenye foleni ya mstari benki au ukiwa umelala kitandani na mpenzi wako mkiwa mnaangalia televisheni.

Wanawake wengi hawajui umuhimu wa hili zoezi mpaka wakishachelewa – na kupata tatizo la kupiga chafya na kuhisi mkojo kidogo kuvuja.

Misuli ya sakafu ya nyonga ni muhimu kwasababu inatoa msaada kwa kibofu na matumbo, ila pia mfuko wa uzazi. Kufanya haya mazoezi, kunasaidia kuweka misuli kuwa imara, ili kuepuka uharibifu wakati wa ujauzito na kujifungua.

Jinsi ya kufanya mazoezi ya sakafu ya nyonga

Inasahuriwa kurudia kukaza na kuachia misuli yako ya sakafu ya nyonga mara nane na ufanye hivyo mara tatu kwa siku, ukiwa unafanya haya mazoezi.

Kaza misuli unayotumia kubana mkojo usitoke.

Shikilia hapo hapo ukiendelea kubana kwa sekunde kadhaa, alafu achia misuli ipumzike.

Bana misuli tena, kwa haraka wakati huu, shikilia kwa sekunde kadhaa, halafu iruhusu irudie hali ya kawaida. Rudia mara nane.

Ni muhimu kukumbuka kuepuka kubana pumzi, kubana makalio, kubana miguu yako pamoja na kubana tumbo lako ndani. Kama una maswali yeyote juu ya jinsi ya kufanya haya mazoezi muulize daktari au mkunga wako kwa msaada wa zaidi.

Mazoezi ya sakafu ya nyonga yanafanya kazi vizuri. Wanawake wanaofanya mazoezi haya mara kwa mara, wanaonekana kupata wakati mrahisi katika kujifungua na kupona mapema.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.