Mazoezi ya Kuepuka Kipindi cha Ujauzito

Wakati mazoezi mengi ni salama wakati wa ujauzito, kuna mazoezi mengine ni ya kuepuka. Baadhi ya haya mazoezi yanabeba hatari ya kudondoka au kujichubua, baadhi yana hatari kwa sababu fulani na baadhi sio salama tu.

Ni muhimu kuepuka:

  • Kulala juu kwa mgongo wako wakati wa mazoezi, kwa sababu hii huweka shinikizo kwenye mishipa ya damu nyuma yako na inaweza kuingiliana na mtiririko sahihi wa damu.
  • Michezo ya kugusana kama vile ndondi, soka, bawa na judo.
  • Michezo ambayo ina hatari ya kuanguka kama vile kuendesha baiskeli.
  • Mazoezi yenye athari kubwa katika mishipa na viungo.

Wakati wa mazoezi, ni muhimu kuvaa brazia ya kuridhisha na kusaidia vizuri matiti yako yanayokua. Jaribu kuvaa brazia zilizotengenezwa na pamba maana zina tabia ya kufyonza jasho. Nguo zenye kubana sana hazina uhuru, kwa hiyo ni vyema kuziepuka.

Mazoezi kwa sana yanaweza kusababisha kujifungua mtoto mwenye uzito hafifu, kwa hiyo ni muhimu kutozidisha mazoezi na kujadiliana mara na kipindi cha mazoezi na daktari wako.

Kwa wanawake wengine haipaswi kufanya mazoezi kwa sababu fulani ambazo ni hatari, zinaweza kuwa na madhara. Baadhi yake ni:

  • Uharibifu wa mimba iliyopita
  • Ukosefu mkubwa wa damu
  • Shinikizo la damu
  • Udhaifu wa kizazi
  • Kutokwa na damu ukeni.
  • Ugonjwa wa moyo au mapafu
  • Kushuka kwa mfuko wa uzazi( mji wa mimba).

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.