Mambo Yanayotakiwa Kufanyika Unapohudhuria Kliniki za Ujauzito

Nani anayetoa huduma?

Kama una afya na unategemea kuwa na ujauzito salama katika miadi yako ya kliniki utahudumiwa na mkunga au manesi maalumu wa afya ya uzazi. Ikiwa una historia ya matatizo ya kiafya, kama shinikizo la damu utapelekwa kwa mtaalamu wa mambo ya uzazi na wajawazito.

Lini nitakua na miadi yangu ya kwanza?

Muda wa miadi yako ya kwanza ya kliniki inategemea na mahali unapoishi. Mara mkunga wako au mshwauri wako wa afya amejua una mimba unaweza kuonana nae mara moja kabla ya miadi mikuu ambayo inaanza wiki ya 10. Katika miadi hii ya kwanza utafahamu kwanini unahitaji foloki asidi na utapewa taarifa muhimu kuhusu kula kwa afya.

 

Maswali nitakayoulizwa na mkunga wangu?

Jiandae kwa maswali mengi na fomu ya kujaza. Mkunga wako anataka kupata ujuzi wa afay yako, ya mpenzi wako na historia ya matibabu ya familia zote mbili.

Baadhi ya vitu utakavyoulizwa ni kama:

  • Tarehe yaa mwisho ya hedhi yako,itamsaidia kujua lini untarajia kujifungua.
  • Kama mimba ilishawahi haribika, kutoa au kama una mtoto,itamsaidia mkunga kujua aina gani ya huduma unahitaji kupewa kipindi chote cha ujauzito.
  • Magonjwa ya kurithi katika familia zenu zote mbili, kama vile kisukari,magonjwa ya moyo, magonjwa ya akili na kansa ya damu. Magonjwa haya yanaweza kurithiwa na kuleta shida wakati wa ujauzito hivyo kuwa muwazi kwa mkunga wako.

Kama una miaka chini ya 25,mkunga atafanya viimo vya ugojwa wa kuambukiza wa klamidia.

  • Kazi yako, kama umeajiriwa na aina ya kazi kwasababu baadhi ya kazi zinahatrisha ujauzito.
  • Maisha yako ya kila siku, mkunga atakuuliza kama unavuta sigara na kunywa pombe, maana yote haya yanaweza athiri afaya ya mtoto.
  • Wapi ungependelea kujifungulia mtoto wako.
  • Faida na haki za wamama wajawazito.
  • Kama unategemea kunyonyesha.

Mkunga wako atatumia taarifa uliyompatia kuamua kama unahitaji huduma ya zaidi kutoka kwa mtaalamu wa afya ya uzazi au la. Pia atakushauri:

  • Kufanya mazoezi wakati wa ujauzito hasa mazoezi ya sakafu ya nyonga
  • Kutumia virutubisho kama foliki aside na vitamin D
  • Kula kwa afya.

Vipimo nitakavyofanyiwa ni kama ifuatavyo:

Vipimo vya damu

Kipimo cha damu kitachukuliwa na kuimwa maabara ilikuangalia viwango vya haemoglobini, kundi la damu na kama damu yako ina wadudu hatari

Screening tests (kipimo cha uchunguzi)
Damu yako itachukuliwa ili kuchunguzwa kama mwanao ana hatari za  kuwa na ugonjwa wa akili (Down’s syndrome) au  tatizo la maumbile yake .

Damu yako itatumika kuchunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi, kaswende,kisonono na homa ya ini.

Kipimo cha mkojo

mkunga atakupa chupa kwaajili ya kuweka mkojo, na kuongeza kemikali kuangalia kama mkojo wako una protini. Katika siku za kwanza za ujauzito, protini katika mkojo wako ni dalili ya matatizo, yakiwepo:

  • UTI
  • Shida ya kibofu
  • Shinikizo kubwa la damu
  • Kisukari

Protini katika mkojo siku za mwisho za ujauzito wako zinaonyesha dalili za kifafa cha mimba. Protini katika mkojo wako mara kwa mara ina maanisha uchafu kutoka ukeni umeingia kwenye mkojo.

Kipimo cha shinikizo la damu
mkunga wako atakupima shinikizo la damu na kuandika kwenye kadi yako ya ujauzito. Shinikizo kubwa la damu wakati wa ujauzito ni tahadhari za awali za dalili ya kifafa cha mimba.

Kipimo cha Ultrasound scan

Ni muhimu kujua mtoto wako anaendeleaje na jinsia yake pale mda utakapofika kama utapenda kujua.

Mara ngapi nitakua na miadi ya kliniki?

Hii inategemea na mahali unapoishi na kama mimba yako ni salama. Baada ya miadi yako ya kwanza ndani ya wiki ya 10, miadi mingine ifanyike:

  • Wiki ya 16
  • Wiki ya 25
  • Wiki ya 28
  • Wiki ya 31
  • Wiki ya 34
  • Wiki ya 36
  • Wiki ya 38
  • Wiki ya 40
  • Wikiya 41, kama mtoto hajazaliwa bado.

Utapewa kipeperushi kinachotoa habari kuhusu nini utegeme na lini kwenye miadi yako. Unaweza kujadiliana na mkunga wako ratiba  hii.

Kama huu ni ujauzito wako wa pili, itakubidi uwe na miadi saba tu,ikiwa mimba yako haina matatizo,miadi hiyo ni katika wiki ya:

  • Wiki ya 16
  • Wiki ya 28
  • Wiki ya 34
  • Wiki ya 36
  • Wiki ya 38
  • Wiki ya 41 kama mtoto hajazaliwa bado.

Ikiwa una wasiwasi na huwezi kusubiria mpaka miadi yako iliyopangwa, wasiliana na mkunga wako upate kuonana nae mapema. Matatizo ya kiafya na matatizo yaliyosababishwa na ujauzito yanasababisha afya ya mama mjamzito iangaliwe kwa ukaribu zaidi na wataalamu wa mambo ya uzazi. Mda mwingi katika miadi hii utaonana na daktari badala ya mkunga, na unaweza kufanyiwa uchunguzi sana kuliko wanawake wajawauzito wengine.

Tatizo mwishoni mwa ujauzito inaweza sababishwa na kupanda kwa shinikizo la damu au chupa ya uchungu kupasuka kabla ya uchungu kuanza hivyo utapelekwa kwenye wodi utakayoangaliwa kwa umakini zaidi.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.