Unaweza ukala kila kitu. Ladha za vyakula zitaingia kwenye maziwa, na watoto wengi wanapenda.
Mara kwa mara mtoto hutenda au kujibu kutokana na kitu kwenye mlo wa mama – vitu vya hatari sana ni maziwa ya ng’ombe na chakula chenye dutu zenye kufanya uvutikaji wa nafaka haswa kwenye ngano. Kama mtoto wako atapata shida kutokana na kitu ambacho umekula wewe ni vyema ukamchunguza kwa makini. Dalili zinaweza kujumuisha kupiga chafya, kinyesi cha kijani chenye ukamasi au damu na kuwashwa au kujaa gesi tumboni. Kuondoa hatari hizo kwenye mlo wako inaweza kuwa ngumu lakini ni vema kujaribu kwa manufaa ya mtoto wako.
Baadhi ya wamama wana wasiwasi kuhusu kutumia kahawa. Kiasi kidogo cha kahawa kinapita katika maziwa na utafiti unaonyesha matumizi ya kahawa yana tofauti kidogo kwa mtoto wako. Kama una mtoto mwenye kuchangamka sana, na mgumu kukabiliana nae, na mwenye kusumbua wakati wa kulala, fikiria kupunguza matumizi ya kahawa kwenye mlo wako(kahawa, vinywaji vyenye wanga, chai, chokoleti n.k).
Je, kunyonyesha kutanisaidia kupunguza uzito?
Wataalamu wengi wa afya wanashauri kula kalori 300 zaidi ya kawaida kwa siku kwasababu kunyonyesha kunahitaji nguvu ya ziada. Kama hutumii nguvu ya ziada, mwili wako utaanza kutumia virutubisho vinavyotumika kutengeneza maziwa, kuunguza dutu za fati zilizohifadhiwa na kusaidia kupunguza uzito. Kwa kawaida kama unanyonyesha ni vyema ukawa unakula wastani wa kalori 2500 kwa siku. Hizi unaweza kuzipata kwa kuhakikisha unakula mlo kamili wenye virutubisho vyote muhimu.