Kujifungua kwa Msaada wa Vifaa Maalumu

Wakati mwingine inaweza ikashindikana kwa mwanamke kumsukuma mtoto wake atoke, anaweza kuwa kwenye madawa au mwenye uchovu mwingi. Kunaweza kukawa na matatizo yanayosababisha anashindwa kumsukuma mtoto, au dharura imetokea na inalazimu kujifungua kufanikiwe kwa haraka.

Chuma za kujifungulia (Forceps)           

Forceps (chuma za kujifungulia) zinatumiaka kushikilia na kuvuta kichwa cha mtoto kilichokwama ndani ya njia ya kujifungulia. Daktari wako anaweza akapasua kidogo uke wako kuongeza njia ya forceps kuweza kupita na baadae kichwa cha mtoto wako. Wakati wa mkazo wa misuli ya mfuko wako wa uzazi ukiwa unasukuma, daktari atavuta taratibu kwa msaada wa forceps. Kwa kawaida kama majaribio matatu ya kumtoa mtoto yatashindikana utahitajika kufanyiwa upasuaji.

 Kifaa utupu cha kuvutia (Ventouse/Vacuum extractor)

Njia hii inatumia kifaa kinachotumia nguvu ya utupu (vacuum). Kikombe chenye utupu kitawekwa juu ya kichwa cha mtoto wako na kuunganishwa kwenye pampu. Baada ya kufanikiwa kukikamata kichwa vizuri kwa nguvu ya utupu, utaratibu kwa kujaribu kumsaidia mama ajifungue ni kama ilivyo kwenye forceps. Pale mama anapopata maumivu ya kusukuma na daktari pia atakuwa anavuta kichwa cha mtoto taratibu. Kama baada ya majaribio matatu kujifungua kumeshindikana, utahitaji kufanyiwa upasuaji wa dharura kuweza kujifungua.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.