Hatua za Ukuaji: Mtoto wa Miezi 2

Hatua mwanao alizofuzu (watoto wengi wanazifikia)

  • Anaanza kutoa sauti, milio ya kitoto na minong’ono.
  • Ataanza kufuatilia vitu kwa macho na kuwagundua watu aliowazoea kwa mbali.
  • Anagundua mkono wake.
  • Atanyanyua kichwa chake juu kwa muda mfupi.

Hatua za ukuaji zinazojitokeza (nusu ya watoto wanazifikia)

  • Kutabasamu,kucheka
  • Kuinua kichwa digrii 45.
  • Kusogeza miguu na mikono taratibu.

Hatua za mapema kabla ya wengine (watoto wachache wanazifikia)

  • Kujiinua unapomlaza tumboni kwako.
  • Kuhimili uzito wake kwenye miguu yake
  • Kukihimili kichwa chake kwa uimara
  • Atajibembeleza mwenyewe kwa kuweka mkono mdomoni.

Ataanza kunung’unika na kusumbua pale anapochoshwa na kitu au mdoli.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.