Hatua za Ukuaji: Mtoto wa Miezi 10

Hatua mwanao alizofuzu (watoto wengi wanazifikia)

  • Anatambaa vizuri
  • Anazunguka na kuchunguza sana
  • Mtoto ataanza kuchunguza vitu katika njia tofauti kama kugongagonga, kutupa na kutikisa

Hatua za ukuaji zinazojitokeza(nusu ya watoto wanazifikia)

  • Anasema mama au baba.
  • Ananyooshea mkono vitu vilivyo mabali.
  • Anaitikia ukimwita na anaelewa maana ya neno HAPANA.
  • Anaonyesha anachotaka kwa kuonyesha ishara.

Hatua za mapema kabla ya wengine (watoto wachache wanazifikia)

  • Anaweza kutumia kikombe mwenyewe.
  • Kusimama mwenyewe kwa sekunde chache.
  • Ataanza kujilisha mwenyewe baadhi ya vyakula kama matunda yaliyokatwa vizuri.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.