Hatua za Ukuaji: Mtoto wa Miaka 5

Mtoto wa umri huu:

  • Anaweza kuvaa mwenyewe isipokuwa kufunga viatu.
  • Anaweza kuruka na kutua na mguu mmoja.
  • Anaweza kutupa mpira na kudaka.
  • Anauliza maswali mengi na ana shahuku.
  • Anaigiza wengine.
  • Anatambua herufi na namba.
  • Anaweza kuiga kuimba nyimbo, hadithi.
  • Anashirikiana na wenzake kwenye michezo.
  • Anasaidia watu nyumbani.
  • Anaelewa hisia za watu wengine.

 

Ukuaji wa kimwili katika umri huu

  • Anakomaa kiakili
  • Anaweza kusimama na mguu mmoja bila kuyumba
  • Anashuka ngazi bila kujishika
  • Anakimbia na kusimama bila kuanguka
  • Anaweza kuruka juu ya matofali na miguu yote bila kuanguka
  • Anaweza kuruka urefu wa hatua tatu na kutua na miguu yote

 

Maendeleo ya mtoto katika jamii ndani ya miezi hii

  • Anapenda kujitegemea lakini bado anatumia mda wake na wazazi wake.
  • Mtoto aliye na miaka 5 anapenda kujihusisha na mengi, na mara nyingi atakataa msaada wako.
  • Wanafanya usafi wenyewe, wakati mwingine bila kuamriwa.
  • Wapenda kubembeleza wenzake hasa kama walihusika katika ugomvi.
  • Wanaweza kujielezea wanavyohisi, mfano “huzuni, hasira, kuchanganyikiwa , uoga,kuvunjika moyo” n.k
  • Wanakua kipaji cha kuwasiliana na kujadiliana na marafiki zake katika michezo yao.
  • Wanaweza kuwa na rafiki mmoja kipenzi.
  • Wana vipaji vingi vya kushirikiana na rafiki zake wengine.
  • Wanashiriki katika kazi za vikundi shuleni na wanaweza kusubiria zamu yao kuongea au kufanya onyesho.
  • Wazazi na walimu ni watu muhimu kwao, na chanzo cha habari na faraja.
  • Wanaanza kufuata kanuni na sheria na wakati mwingine wanakumbusha wenzao, bila maelekezo ya mwalimu au mzazi.

 

Hatua za ukuaji katika kuongea na kujifunza

  • Wanaelezea mahitaji, hisia, na mawazo yao.
  • Wanapenda kupata habari zaidi.
  • Wanafanya suluhisho la matatizo na kuchunguza mawazo yao.
  • Wanafanya mipango ya vitu wanavyohitaji.
  • Wanashauri wenzao na kutetea mada.
  • Wanatengeneza na kuhadithia hadithi.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.