Fahamu Matunzo Muhimu ya Mtoto kwa Ujumla

Matunzo kwa mtoto wako yanafurahisha, yanachosha na ni yenye hisia nyingi. Hapa tutakupa mbinu mbalimbali za kuweza kufanikiwa kumaliza wiki ya kwanza na kuendelea safari yako ya malezi.

Ngozi

Ngozi ya mtoto wako ni laini sana. Wiki za mwanzoni utaweza kuona chunusi za utotoni na vidoti doti vyeusi. Kila siku mchunguze mtoto wako juu mpaka chini. Chunguza mikunjo wa kwenye shingo, nyuma ya masikio, kwenye kwapa na sehemu zake za siri (Chunguza korodani kwa makini kama mtoto ni wa kiume). Mara nyingi uchafu na ngozi iliyokufa hujazana katika mikunjo hii ya ngozi na huweza kusababisha maambukizi kama “candida” kama hazitafanyiwa usafi vizuri.

Sehemu za siri za mtoto

Unaweza ukagundua kwamba sehemu za siri za mtoto wako zimevimba na kuwa nyekundu. Hii ni kawaida katika wiki kadhaa za mwanzo, na hutokana na kuwepo mda mrefu sehemu yenye homoni za ujauzito.

Kama dalili hizi hazitatoweka ndani ya wiki sita za mwanzo, ni vyema kumshirikisha mtoa huduma za afya utakapoenda kliniki.

Uume uliotahiriwa

Kuhudumia uume uliotahiriwa ni rahisi, unachotakiwa kufanya ni kuhakikisha ngozi ya uume ni safi na sehemu yenye kidonda inaachwa kavu mpaka itakapopona. Wiki chache za mwanzo baada ya kutahiriwa uume utaonekana kuvimba na wenye maumivu ukiguswa.

Uume usiotahiriwa

Wakati wa kumuosha au kumuogesha mtoto ambaye hajatahiriwa, usijaribu kuirudisha ngozi ya mbele ya uume (govi) ili usafishe chini yake. Osha nje ya uume kama ambavyo unaosha sehemu nyingine ya mwili.

Kutegemea na mtoto wako, inaweza kuchukua wiki, miezi hadi miaka kwa ngozi ya mbele ya uume wake kujitenga na uume wake ili iweze kubenjuka kwa nyuma. Kwa sasa usilazimishe.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.