Hatua za Ukuaji: Mtoto wa Mwaka 1

Hongera! Mtoto wako sasa si kichanga tena, na ametimiza mwaka mmoja.

Hatua mwanao alizofuzu (watoto wengi wanazifikia)

  • Anaigiza kazi za watu wengine kama kupika,kuongea na simu-mara nyingi anaigiza kile alichoona wewe na mwezi wako mnafanya.
  • Kupiga makofi, kuaga na kuonyesha kitu kwa kidole.
  • Kutumia ishara muhimu kama kutikisa kichwa akisema hapana au kupungia mkono akiaga.

Hatua za ukuaji zinazojitokeza (nusu ya watoto wanazifikia)

  • Kuitikia na kuelewa maswali rahisi utakayomuuliza na uelekeo mfano: njoo hapa.
  • Atasema maneno kama “mama” au “baba” na mishangao kama”aaah, ooho”
  • Mtoto ataanza kutembea hatua chache bila kushikwa na mtu.
  • Kusimama mwenyewe.
  • Wanatambua vitu na kukiangalia mara utakapokitaja.

Hatua za mapema kabla ya wengine (watoto wachache wanazifikia)

  • Kutembea vizuri
  • Kutumia vitu sawa kama kunywa maji kutumia kikombe, kuchana nywele kwa chanuo.
  • Mtoto kuelewa maneno kama kunywa, gari au mpira.
  • Anasema maneno mengine mawili ukiachana na mama na baba.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.