Matatizo ya Usingizi kwa Mtoto

Omba msaada kama unajisika mambo hayaendi vizuri

Wazazi wengi wanapata shida kuwafanya watoto wao walale. Hata kama mambo yalikua yanaenda vizuri, muda fulani matatizo ya kulala yanakuja. Baadhi ya matatizo yanaweza kuanza kwasababu ya suala la kimwili, kama kutoka maziwa bila kutegemea. Muda mwingine kitu cha kihisia kinaweza msababisha mtoto kulia katikati ya usiku. Mfano mtoto wa miezi kumi anaweza kuamka kila mara wakati wa usiku kwasababu ya hofu ya kuachwa wakati mama yake anaenda kazini.

Kama mtoto wako ana matatizo ya kulala na kujisikia kutokuwa sawa, omba msaada. Daktari wa mtoto wako anaweza kuwa msaada mkubwa. Anaweza kudhibiti tatizo, kama kutokucheua au kucheua sana au matatizo mengine ya mfumo wa chakula na kukupatia maoni yenye kukusaidia mtoto wako apumzike vizuri.

Unaweza pia kupata ushauri kutoka kwa majirani zako ambao wana watoto wakubwa, na kujifunza ni yapi walifanya kipindi wakiwa na tatizo kama lako.

Ni muhimu kwa wazazi wa mtoto kuwajibika pamoja kama mtoto wao ana matatizo ya kupata usingizi. Kama mtoto wako ana usingizi wa shida ina maana na wewe pia utakuwa na shida hiyo. Ni hali ya asili kuwa na hasira katika kipindi hiki. Jaribu kuwa makini kwenye hili tatizo na kuwajibika pamoja na mwenza wako. Ikiwa wote mtakua pamoja na kusaidiana, mambo yanaweza kuwa rahisi.

Programu ya AfyaTrack

Programu ya kwanza nchini Tanzania ya kufuatilia maendeleo ya ujauzito na ukuaji wa mtoto kwa lugha ya Kiswahili.